Atiwa Mbaroni Kwa Kukutwa na laini za simu 141 zenye usajili wa majina ya watu wengine.

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linamshikilia mtu mmoja MWAKILA S/O ALLY [32], mkazi wa Mwambene, Jijini Mbeya  kwa tuhuma za kupatikana na laini za simu [141] zenye usajili wa majina ya watu wengine.
 
Mnamo tarehe 12/07/2019 majira ya saa 13:00 mchana huko mtaa wa Itongo kata ya Mwambete tarafa ya Iyunga. Mtuhumiwa ambaye pia ni fundi umeme baada ya kukamatwa na kuhojiwa alikiri kumiliki laini hizo za simu 141 za mitandao tofauti zilizosajiliwa kwa majina tofauti ikiwemo “HALOTEL” laini 13, TIGO laini 29, TTCL laini 01, VODACOM laini 78 na AIRTEL laini 20. Pia alikutwa akiwa na vocha zilizotumika  za Vodacom 05, Tigo 04, Airtel 48, Halotel 03 pamoja na simu Itel 03, “Oking” 01 na “Hotwave” 01.
 
Chanzo ni kujipatia kipato. Mtuhumiwa atafikishwa Mahakamani mara baada ya upelelezi kukamilika.
 
       Imetolewa na:
[ULRICH O. MATEI – SACP]
KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments