POLISI KILIMANJARO WAKAMATA NDOO 60 ZA SAMAKI WACHANGA BWAWA LA MUNGU

Polisi mkoani Kilimanjaro wamekamata ndoo 60 za samaki wanaodaiwa kuvuliwa kinyume cha sheria katika Bwawa la Nyumba ya Mungu wilayani Mwanga  wakiwa wanafirishwa kwenda Arusha.



Samaki hao wamekamatwa leo Juni 18 majira saa tisa usiku katika kata ya Lag’ata wilayani Mwanga ambapo Kamanda wa polisi wa Mkoa huo, Hamis Issah, amewambia wandishi wa habari kuwa samaki hao walikamatwa wakiwa kwenye aina ya Mistubishi pajero yenye namba za usajili T. 527  AEQ na kwamba wanawashikilia watuhumiwa wawili waliokutwa na samaki hao.

Amewataja watuhumiwa hao ni mfanyabishara Godlisen Mfinanga (37), mkazi Mrombo Arusha na Mwidini Seleman (30) mkazi wa kisongo Arusha na kwamba watafikishwa Mahakamani.



Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527