NAPE AMMWAGIA PONGEZI WAZIRI MAKAMBA


Mbunge wa Jimbo la Mtama,Nape Nnauye ametoa pongezi kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira kwa kusimamia suala la katazo la mifuko ya Plastiki.


Katika ukurasa wake wa Twitter leo asubuhi Jumatatu Juni 3, 2019 Nape ameandika ujumbe akisema kazi iliyofanywa na Makamaba ni mfano wa kiongozi na siyo mtawala .

Akiwa ameambatanisha picha yake (Nape) na Makamba wakiwa wamevalia masharti ya rangi ya kijana inayotumiwa na CCM, Nape amendika, “Namna wewe na wenzako mlivyosimamia swala la mifuko ya plastiki ni mfano tosha wa utofauti kati ya kuongoza na kutawala.. Hongera sana!.”

Waziri Makamba ameongoza kampeni hiyo ikiwa ni utekelezaji wa agizo la Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alilotoa bungeni miezi kadhaa iliyopita akisema kuanzia Juni mosi, 2019, itakuwa ni marufuku kutengeneza, kuingiza, kuuza na kutumia mifuko ya plastiki kwa ajili ya kubebea bidhaa za aina yoyote na matumizi yake yatakoma Mei 31, 2019.



Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post