MWENYEKITI WA CHAMA CHA UMMA (CHAUMMA) HASHIM RUNGWE ARIPOTI POLISI

Mwenyekiti wa Chama cha Umma (Chaumma) Hashim Rungwe ameripoti katika kituo cha polisi Osterbay kuitikia wito wa kamanda wa polisi Mkoa wa Kinondoni Mussa Taibu.


Rungwe amefika kituoni hapo saa 4.10 asubuhi ya leo Jumatatu Juni 3, 2019  akiwa amevalia kanzu nyeupe akiongozana na mtu mmoja ambao wote wameingia katika ofisi ya Kamanda Taibu.

Mwenyekiti huyo amefika kituoni hapo baada ya jana Jumapili Eugene Kabendera, kwa niaba ya Sekretarieti ya Ushirikiano wa Vyama nane vya Upinzani kutoa taarifa akisema polisi walifika katika ofisi za Chaumma jijini Dar es Salaam na kueleza Rungwe anatakiwa kuripoti leo Jumatatu Juni 3,2019 katika ofisi za Kamanda Taibu.

Katika mkutano huo, viongozi wa vyama hivyo walitoa tamko la kutoshiriki kwenye uchaguzi wa marudio kwenye kata 32 unaotarajiwa kufanyika  Juni 15, 2019 kwa sababu unasimamiwa na Wakurugenzi Halmashauri za wilaya na Manispaa kinyume na uamuzi wa Mahakama Kuu.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post