MAREKANI KUTUMA ASKARI 1,000 MASHARIKI YA KATI KUIKABILI IRAN


Serikali ya Marekani imesema itatuma askari 1,000 zaidi kwenye avikosi vyake vilivyopo Mashariki ya Kati kufuatia kushamiri kwa sintofahamu na taifa la Iran.


Taarifa iliyotolewa na Wizara ya Ulinzi ya Marekani, The Pentagon, imeeleza kwamba Ikulu ya Marekani na Kamati ya Wakuu wa Vikosi vya ulinzi na Usalama tayari imekwisha ridhia kupelekwa kwa askari wa majini, ardhini na anga watakao fikia 1,000 ili kuongeza nguvu zaidi kwa vikosi vilivyopo.

Kaimu Waziri wa Ulinzi Patrick Shanahan, amenukuliwa akisema kwamba nyongeza ya askari hao inafuatia kushamiri kwa vitendo vya chuki na uhasama vinavyo fanywa na serikali ya Iran hivyo kuhatarisha maslahi ya Marekani na Washirika wake Mashariki ya kati.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post