BARABARA ZAFUNGWA MOSHI IBADA YA MAZISHI YA DR. MENGI

Haijapata kutokea. Ndivyo unavyoweza kusema kutokana na umati wa watu waliojitokeza katika ibada ya mazishi ya aliyekuwa Mwenyekiti wa Kampuni za IPP, Reginald Mengi.

Barabara zote za kuingia na kutoka katika Kanisa Kuu la Usharika wa Moshi mjini wa Dayosisi ya Kaskazini ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), zimefungwa kwa kuwekewa utepe wa njano na polisi.

Barabara ya kuelekea kanisa hilo ukitokea ofisi ya mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro imefungwa kuanzia jengo la NSSF Commercial Complex, wakati ile ya kutokea barabara ya Boma kuelekea kanisani imefungwa kuanzia ilipo benki ya KCB.

Na Daniel Mjema, Mwananchi

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527