MAMIA YA WAOMBOLEZAJI WAJITOKEZA KUSHIRIKI IBADA YA MAZISHI YA REGINALD MENGI


Mamia ya waombolezaji leo Alhamisi Mei 9, 2019 wamejitokeza katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Usharika wa Moshi Mjini kushiriki ibada ya mazishi ya aliyekuwa mwenyekiti wa Kampuni za IPP, Dr. Reginald Mengi.



Baadhi ya waliofika kanisani hapo ni mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, James Mbatia, mbunge wa kuteuliwa, Anne Kilango  na mbunge wa Mtama (CCM), Nape Nnauye.

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa  ndo ataongoza ujumbe wa Serikali katika mazishi ya Mengi aliyefariki dunia usiku wa kuamkia Mei 2, 2019 Dubai, Falme za Kiarabu.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527