BABA AFIKISHWA MAHAKAMANI KWA KUBAKA MTOTO WAKE

Said Rashid (36), mkazi wa Mbezi Juu jijini Dar es Salaam amefikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Kinondoni akikabiliwa na shtaka la kumbaka mwanaye mwenye umri wa miaka 13.

Akisoma hati ya mashtaka jana Jumatano Mei 29, 2019 mbele ya hakimu, Anifa Mwingira, wakili wa Serikali, Matarasa Hamisi amedai kati ya mwaka 2016 na 2019 mshtakiwa alimbaka mtoto wake huku akijua kufanya hivyo ni kosa la kisheria.

Matarasa amedai upelelezi wa kesi hiyo haujakamilika na kuomba mahakama kupanga tarehe nyingine ya kutajwa.

Wakati mshtakiwa huyo akikana kufanya kitendo hicho Hakimu Mwingira alieleza kuwa dhamana ipo wazi, akimtaka kuwa na wadhamini wawili wanaotambulika kisheria watakaosaini bondi ya Sh1 milioni kila mmoja.

Hata hivyo, mshtakiwa alishindwa kutimiza masharti ya dhamana na kupelekwa rumande hadi Juni 10, 2019.

Na  Pamela Chilongola, Mwananchi 

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527