AUNTY EZEKIEL AWAVAA WANAOHOJI KUHUSU MPENZI WAKE


Staa wa Bongo movie, Aunt Ezekiel amewataka wanaofuatilia mahusiano yake kumwachia mwenyewe, huku akidai suala la yeye kuwa na wanaume aliowazidi umri kwake si tatizo.

Aunt Ezekiel amesema amekuwa akikutana na maneno mengi, huku wengi wakidai amekuwa na tabia ya kutembea na wanaume wadogo kuliko umri wake, kitu ambacho kwake haoni tatizo, kwa kuwa wengi hawajui hayo ni maisha binafsi ya mtu.

“Suala la mimi kutembea na wanaume wadogo sidhani kama linatakiwa liingiliwe, haya ni maisha binafsi ya mtu, najua kila mmoja ana aina ya maisha anayotaka aishi, nadhani sipaswi kuingiliwa katika hili zaidi ya watu kushabikia kile ninachofuata,”alisema Aunt.

Kwa sasa inadaiwa staa huyo ameachana na baba wa mtoto wake, Mose Iyobo, ambaye ni mnenguaji wa lebo ya WCB, ambao walijaliwa kupata mtoto aitwaye Cookie.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527