AJALI YA HIACE YAUA WATU 7 NA KUJERUHI 12 KIGOMA

Watu 7 wamefariki dunia na wengine 12 kujeruhiwa baada ya gari walilokuwa wakisafiria kupasuka tairi la nyuma na kupinduka mkoani Kigoma.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kigoma, Martin Ottieno amesema ajali hiyo ilitokea jana saa 12 :15 jioni katika kijiji cha Mlela wilayani Uvinza mkoani humo.

Alisema gari hiyo iliyokuwa inatokea wilayani Uvinza kwenda Kigoma mjini ilipasuka tairi la nyuma upande wa kushoto na kupinduka.

Majeruhi wote wamepelekwa Hospitali ya Mkoa ya Maweni.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527