JAMAA AKAMATWA NDANI YA KANISA LA MTAKATIFU PATRICK AKIWA NA PETROLI NA KIBERITI

Kanisa la Mtakatifu Patrick lilijengwa karne ya 19

Mwanaume mmoja amekamatwa baada ya kuingia kwenye kanisa la Mtakatifu Patrick jijini New York akiwa amebeba makopo mawili ya Petroli, kibiriti , Polisi anaeleza.

Walinzi walimkabili mtu huyo mwenye miaka 37 alipokua akiingia kanisa la Manhattan siku ya Jumatano jioni.

Aliyamwaga mafuta chini kisha maafisa wakamkamata kumpeleka korokoroni.

Naibu kamishna wa polisi John Miller amesema tukio hilo linaloshukiwa kuwa baya lilitokea siku mbili baada ya kanisa la Notre-Dame jijini Paris.

''Mtu alikua akitembea usawa wa kanisa amebeba magaloni ya mafuta, na vibiriti, ni jambo la kushukiwa''.Alisema Bwana Miller

Afisa wa intelijensia na masuala ya ugaidi amesema ni 'mapema sana' kueleza kama kusudio la mtu huyo ni kutekeleza vitendo vya kigaidi

Alipokabiliwa nje ya Kanisa, Mwanaume huyo aliwaambia maafisa kuwa gari yake iliishiwa mafuta na alikua akipita mbele ya kanisa hilo ili kulifikia.Alikamatwa na polisi walitazama gari lake na kuona kuwa halikua limeishiwa mafuta.

Haijulikani mtu huyo alikua na mipango gani.
Chanzo - BBC

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post