MBUNGE WA CCM AFUNGUKA BAADA YA NDOA YAKE KUVUNJIKA



Mbunge Bonnah Kaluwa

Mbunge wa Segerea (CCM) jijini Dar es Salaam aliyekuwa akitumia jina la Bonnah Kaluwa amekiri kuachana na mume wake Moses Kaluwa na hivyo kulazimika kubadili majina yake ya mwisho.

Mbunge huyo wa CCM ambaye katika mitandao yake ilikuwa ikifahamika kwa jina la Bonnah Kaluwa sasa yanasomeka kama 'Bonnah Kamoli'.

Hata hivyo baada ya tetesi hizo kusambaa kwa kasi, kupitia gazeti linalotoka kila siku Bonna amekiri ukweli wa taarifa hizo.

“Taarifa ni za kweli tumeachana. Ni matatizo ya kifamilia. Nimeshaweka majina yangu kwenye mitandao ya kijamii. Nimeweka Instagram, Facebook. Bunge wana taratibu zao, si wamepata barua", amesema Bona.

Hata hivyo tovuti ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania bado imeendelea kutumia majina yake ya awali ya ‘Bonnah Moses Kaluwa'.
Chanzo - EATV

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527