NDEGE YAANGUKA NA KUUA WATU WATANO KENYA

 Watano wamefariki dunia leo Jumatano Februari 13, 2019 baada ya ndege ndogo waliyokuwa wanasafiria kuanguka katika kaunti ya Kericho nchini Kenya.

Ndege hiyo ilianguka kwenye msitu wa Londiani ikiwa na abiria watano, mkuu wa kikosi cha anga, Kamanda Rodgers Mbithi amesema abiria wote waliokuwa kwenye ndege hiyo wamefariki dunia.

Amesema waliopoteza maisha katika ndege hiyo Cesna 206-5-Y BSE ni wanaume watatu na wanawake wawili ambao hawajatambulika ni raia wa nchi gani.

Kwa mujibu wa kamanda wa kaunti ya Londiiani, Justus Munyao, ndege hiyo inamilikiwa na kampuni ya Safari ambayo huchukua abiria kutoka Ol Kiombo kuelekea Kaunti ya Turkana.

Amesena tukio hilo lilitokea saa 5 asubuhi kwenye msitu wa Masaita.

Kamanda wa Kikosi cha Rift Valley, Edward Mwamburi amesema polisi wameshafika eneo la tukio.
Via Mwananchi

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527