MABAHARIA "ORIGINAL" WALIA JINA LAO KUTUMIKA KIHUNI



Chama cha mabaharia nchini kimeitaka jamii kuondokana na dhana potofu za kuonekana mabaharia ni wahuni na badala yake waiheshimu taaluma hiyo kama zingine.

Akizungumza na Habari xtra ofisini kwake mwenyekiti wa Chama hicho Frank Chuma amesema kutokana na jina lao kutumika vibaya miongoni mwa Vijana hali hiyo imesababisha taaluma yao kukosa heshima pindi wanapokwenda katika taasisi nyingine kutafuta huduma. 

Mwenyekiti huyo amesemabado wanakabiliwa na changamoto ikiwemo kutokupata ajira na kanuni zilizopo katika kazi hiyo kuwa kandamizi.

Chanzo -Times fm

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527