RIPOTI YA HAKI ZA BINADAMU ZAIMULIKA SAUDIA NA CHINA

Saudia na China zamulikwa katika ripoti ya dunia ya haki za binadamu

Shirika la Kimataifa la kutetea haki za kibinadamu la Human Rights Watch limekosoa ukiukaji wa haki za binadamu nchini Saudi Arabia na China katika ripoti yake ya dunia ya mwaka 2019, yenye kurasa 400.

Ripoti hiyo pia inazikosoa nchi za Ulaya, lakini Mkurugenzi wa shirika hilo nchini Ujerumani Wenzel Michalski anasema licha ya yote hayo kuna sababu ya kuwa na matumaini kidogo.

Shirika la Human Rights Watch limekuwa likichapisha ripoti hiyo kila mwaka tangu mwaka 1989, mataifa yenye uongozi wa kidikteta ambayo haki za watoto, wanawake na wanaume zinakiukwa ndiyo yanayolengwa.

 Mwaka huu kama anavyosema Wenzel Michalski wanaharakati wa haki za binadamu hawajajikita tu katika baadhi ya nchi kwa ujumla bali kwa watu binafsi.

China inajaribu kuiuza sera yake ya ukiukaji wa haki za binadamu duniani

Chanzo:Dw

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527