TUNDU LISSU : NIPO TAYARI KUGOMBEA URAIS TANZANIA

Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema) Tundu Lissu ameendelea kusimamia msimamo wake kuwa yupo tayari kugombea urais mwaka 2020 endapo chama chake kitaona anatosha kusimama katika nafasi hiyo.

Akihojiwa na Shirika la utangazaji la Uingereza (BBC) Lissu amesema kauli hiyo haina maana yoyote kwamba anapambana na Edward Lowassa ambaye alisimamishwa na Chadema mwaka 2015 kuwania nafasi hiyo.

“Kama chama changu pamoja na vyama tunavyoshirikiana navyo na Watanzania wanaotuunga mkono watasema kwamba mimi nafaa kuwawakilisha nitakuwa tayari kufanya hivyo.

Alisema, “Sina mpambano na Lowassa uamuzi wa kugombea urais sio wangu wala Lowassa wala Mbowe ni vikao vya chama. Inaweza kwenye vikao viongozi nikaambiwa sitoshi nitakubali na inawezekana vikao vikamwambia Lowassa aniachie mimi nipambane kwa sababu mapambano ya sasa yanahitaji nguvu inawezekana kabisa”.

Kuhusu kwamba ni lini atarejea nchini alieleza, “Daktari wagu atakaposema sasa una uwezo wa kurudi kwenu nitarudi Tanzania.

Lissu alieleza kuwa licha ya kwamba hadi sasa Serikali imeshindwa kufanya uchunguzi na kuwabaini waliomshambulia atarudi na itawajibika kumlinda kwa saa 24.


Na Elizabeth Edward,Mwananchi

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527