FAINALI 7 ZA KIBABE ZILIZOAMULIWA NA RONALDO


Cristiano Ronaldo katika matukio mbalimbali.

Baada ya kufunga bao la ushindi jana katika fainali ya Kombe la Italia, mshambuliaji wa Juventus Cristiano Ronalado sasa amefunga mabao 8 katika fainali 7 zilizopita.

Ronaldo mwenye umri wa miaka 33, jana usiku aliiwezesha timu yake kutwaa taji la Copa Italia kupitia bao lake alilofunga dakika ya 61 dhidi ya AC Milan huku Juventus ikifikisha makombe 8 ya Italia na kuwa ndio klabu iliyoshinda mara nyingi zaidi ikiipiku AC Milan yenye mataji 7.

Fainali ambazo Ronaldo amefunga mabao

Ronaldo alifunga mabao mawili kwenye fainali ya Ligi ya mabingwa Ulaya msimu wa 2016/17 Real Madrid ikishinda 4-0 dhidi ya Juventus.

Ronaldo pia alifunga bao 1 kwenye ushindi wa 2-1 iliopata Real Madrid dhidi ya Barcelona kwenye fainali ya 'Spanish Super Cup'.

Ronaldo pia amefunga jumla ya mabao 4 katika fainali mbili tofauti za Klabu bingwa ya Dunia. Alifunga mabao mawili dhidi ya Kashima Antlers mwaka 2016. Pia akafunga mabao mawili dhidi ya Gremio mwaka 2017.

Bao lake la jana limekuwa bao la nane katika fainali 7 zilizopita huku fainali zote timu alizokuwa akizichezea yaani Real Madrid na Juventus zimetwa ubingwa.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527