Maajabu : KUTANA NA MTU HUYU ANAMALIZA MARA 50 BILA KUFANYA TENDO LA NDOA


Msichana Amanda Gryce, mkazi wa Florida nchini Marekani, anasumbuliwa na ugonjwa ambao sio wa kawaida, unaomfanya afikie mshindo takriban mara 50 kwa siku, bila ya kufanya tendo la ndoa na mtu yeyote.

Msichana huyo mwenye miaka 22, anasema alianza kugundua ana tatizo hilo akiwa na miaka 6, na amekuwa akikabiliana nalo bila kujua hatma yake ni nini, na amekuwa akikutwa na hali hiyo muda wowote na mahali popote bila kufanya tendo la ndoa.

“Ilitakiwa iwe ni kitu kizuri kama ambavyo inatakiwa, imekuwa maumivu kwangu, kwa sababu inatokea sana, inaweza ikatokea hata mara 50 kwa siku au mara tano mpaka kumi kwa saa moja, inatokea nikiwa na rafiki zangu, au nikiwa sehemu tu na watu wengine, nikipanda gari ndio inazidi kutokana na mtikisiko wake, ni aibu sana”, amesema Amanda.

Tatizo hilo ambalo mwenyewe anadai limekuwa likimtesa maisha yake yote na kumfanya asifurahie maisha ya kimapenzi, kilimfanya awahi kuwaza kujiua, lakini mpenzi wake Stuart Triplett, amekuwa akimpa ushirikiano sana wa kutafuta tiba na kumfanya awe na tumaini.

Kutokana na hali hiyo, Amanda ameshakutana na baadhi ya madaktari kujaribu kupata tiba, lakini mpaka sasa hajapata ufumbuzi kutokana na ugonjwa huo kutokuwa na tiba ya moja kwa moja, hivyo kumpa njia mbadala za kukabliana nao, ikiwemo kufanya mazoezi.

Tatizo hilo kitaalamu linajulikana kama 'Persistent Genital Arousal Disorder'ambalo hutokea mara chache sana kwa binadamu. Mpaka sasa haujajulikana tiba sahihi ya kuweza kumaliza tatizo hilo, lakini madaktari wa masuala hayo wameshauri iwapo mtu atagundulika kuwa na tatizo hilo, atatakiwa kuhudhuruia tiba ya mwili 'Physiotherapy'.
Amanda akiwa na mpenzi wake Stuart Triplett

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527