RADI YAJERUHI WANAFUNZI 14 MULEBA

Wanafunzi 14 wa shule ya sekondari Rulongo wilayani Muleba Mkoa wa Kagera wamelazwa katika hospitali ya Lubya wilayani humo baada ya kujeruhiwa na radi.

Akizungumza jana Jumatano Januari 16, 2019 mganga mkuu wa hospitali hiyo, George Kasibante amesema tukio hilo limetokea leo na kwamba kati ya wanafunzi hao, watatu wana hali mbaya baada ya kuungua sehemu kubwa mwilini.

Amesema mwanafunzi mmoja amepoteza fahamu na madaktari wanajitahidi kuhakikisha anarejea katika hali yake ya kawaida, kwamba wengine walipata zaidi mshtuko.

Amesema radi hiyo ilipiga vyumba vya madarasa ya kidato cha pili na tatu, kwamba shule hiyo ipo mlimani eneo ambalo radi hupiga zaidi na kuwashauri wanafunzi kutojikinga na mvua katika maeneo yenye miti mirefu.


Na Shaaban Ndyamukama, Mwananchi

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527