KABURI LAFUKULIWA..SANDA YACHOMWA MOTO SINGIDA


Taharuki katika kitongoji cha Kipondoda wilayani Manyoni mkoani Singida baada ya kaburi moja ambalo linadaiwa kuzikwa mtu siku tano zilizopita na kukutwa limefukuliwa huku sanda ikiwa imechomwa moto upande wa miguuni.

Mwajiri wa marehemu ambaye alishiriki maziko ya ndugu huyo, amesema marehemu Jamal Mkumbo alizikwa Desemba 25, mwaka 2018 kwa kufuata tararibu zote lakini ameshangazwa kukuta kaburi limefukuliwa na sanda kuchomwa moto kutokana nakudaiwa kuwa inawezekana ni imani za kishirikina.

Kwa upande wake mwenyekiti wa kitongoji hicho bw. Jackson Job amekiri kutokea kwa tukio hilo na wamekemea tabia za aina hiyo.

Matukio ya makaburi kufukuliwa wilayani Manyoni yamekuwa yakitokea mara kwa mara na kudaiwa wanaofanya hivyo wamekuwa wakijihusisha na imani za kishirikina.
Chanzo - EATV

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527