UHAMIAJI YAELEZA SABABU ZA KUWAKAMATA WAANDISHI WA HABARI WA CPJ


Idara ya Uhamiaji nchini Tanzania, imetaja sababu ya kuwakamata na kuwashikilia kwa muda waandishi wa habari kutoka Kamati Maalum ya Kuwatetea waandishi wa habari duniani (CPJ).

Pamoja na kuwaachia huru, idara hiyo imesema inaendelea kushikilia hati zao za kusafiria kwa uchunguzi zaidi.

Akizungumza na Mwananchi leo Alhamisi Novemba 8, 2018 Msemaji wa Idara ya Uhamiaji, Ally Mtanda amesema, ‘’ni kweli idara yetu iliwakamata waandishi hao katika maeneo ya hoteli waliyofikia na kufanya nao mahojiano, kwa sababu tulifanya uchunguzi na kubaini wanaenda kinyume na masharti yaliyoainishwa katika madhumuni ya ujio wao hapa nchini.”

Mtanda amesema, waandishi hao Angela Quintal na Muthoki Mumo waliingia nchini Oktoba 31, 2018 kupitia Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, jijini Dar na katika madhumuni ya safari yao walisema wanaingia nchini kwa matembezi ya kawaida na viza yao ilikuwa inafikia ukomo Januari 1, 2019.

SOMA ZAIDI HAPA

Via Mwananchi

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527