RAIS WA KWANZA MWANAMKE ACHAGULIWA ETHIOPIA

Wabunge nchini Ethiopia wamemchagua Sahle-Work Zewde, kuwa rais wa kwanza mwanamke baada ya aliyekuwa rais wa nchi hiyo, Mulatu Teshome, kujiuzulu ghafla leo.


Sahle-Work ni mwanadiplomasia mwenye uzoefu ambaye sasa amekuwa kiongozi wa kipekee mkuu mwanamke barani Afrika.


Kuchaguliwa kwake katika wadhifa huo, kunajiri wiki moja baada Waziri Mkuu, Abiy Ahmed, kuliteua baraza la mawaziri ambapo nyadhifa nusu katika baraza hilo zimewaangukia wanawake.


Katika hotuba yake ya kukubali wadhifa huo, Rais Sahle-Work, amezungumza kuhusu umuhimu wa kudumisha amani.


Rais Sahle-Work amewahi kuwa Balozi wa Ethiopia nchini Senegal na Djibouti na amewahi kushika nyadhifa kadhaa katika Umoja wa Mataifa ikiwamo Mkuu wa Kujenga Amani katika Jamhuri ya Afrika ya Kati.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527