DARAJA REFU ZAIDI CHINA LAZINDULIWA
Rais Xi Jinping wa China leo, Jumanne amezindua daraja refu zaidi lililojengwa na kusanifiwa kwa miaka 15 na lenye urefu wa kilomita 55 huko Zhuhai, kusini mwa China.
Uzinduzi rasmi wa daraja hilo la Hong Kong-Zhuhai-Macao unadaiwa kuwa mradi uliochukua muda mrefu na uliokabiliwa na ugumu zaidi kwani umevuka bahari na ni mradi wa kwanza kujengwa mkoani Guangdong, Macao na Hong Kong.
Daraja hilo limefanikisha azma yake kwa mara ya kwanza katika kuunganisha barabara kati ya Zhuhai, Macao na Hong Kong, huku likipunguza muda wa usafiri kutoka Hong Kong hadi Zhuhai na Macao kutoka saa 3 hadi dakika 45.
SOURCE:AZAM TV