AFIKISHWA MAHAKAMANI KWA KUMCHAPA FIMBO MTOTO

MKAZI wa Mikocheni A, Pyana Herbo (45), amepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Mwanzo Kinondoni, Dar es Salaam kwa tuhuma za kumshambulia kwa mchapa fimbo mtoto.

Karani wa Mahakama hiyo, Januari Kasekwa alidai mbele ya Hakimu Marko Mochiwa kuwa Septemba 10 saa 4 asubuhi eneo la Mikocheni A, Wilaya ya Kinondoni, mtuhumiwa alimshambulia mtoto Christina Hebron kwa kumpiga na fimbo sehemu mbalimbali za mwili.

Mshtakiwa alikana shtaka hilona alirudishwa rumande kwa kushindwa kutimiza masharti ya dhamana hadi Oktoba 5, mwaka huu, kesi itakapotajwa tena.

Na ZAKIA NDULUTE (UoI) Na HAPPYNESS GRAYSON (UoI) | 
Chanzo- Mtanzania

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527