MGAMBO WAKAMATWA NA POLISI KWA KUMJERUHI KWA KIPIGO MFANYABIASHARA DAR

Jeshi la Polisi Mkoa wa Kinondoni linawashikilia mgambo watatu wa manispaa ya Kinondoni kwa tuhuma za kumjeruhi mfanyabiashara, Robson Orotho mkazi wa Bunju jijini Dar es salaam  leo Ijumaa Agosti 31, 2018.

Inaelezwa kuwa mgambo hao walimshushia kipigo mfanyabiashara huyo kutokana na kushindwa kulipa Sh50,000 ya taka.

Kamanda wa polisi wa mkoa huo, Jumanne Murilo amesema watuhumiwa hao wamekamatwa kutokana na kusambaa kwa taarifa zikiwaonyesha wakikiuka sheria za nchi.


"Ni kweli tunawashikilia watuhumiwa watatu kwa kitendo walichokifanya, tumegundua ziko taratibu na sheria zilizokiukwa,watuhumiwa ni Kelvin Edson, Gudluck Festo na Rehema Nyange ambao wote ni mgambo wa manispaa ya Kinondoni"alisema Muliro.

Advertisement

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527