Balaa!! FISI WATAFUNA NG'OMBE WAWILI NDANI YA DAKIKA 45 MWANZA


Wakazi wa kitongoji cha Chang’ombe kijiji cha Iligamba, halmashauri ya wilaya ya Buchosa Mwanza wamejawa na taharuki baada ya fisi kuvamia katika makazi yao na kutafuna ngómbe wawili kijiji hapo.

Tukio hilo limetokea usiku wa kuamkia leo Jumatatu Juni 5,2018 saa nane usiku ambapo fisi hao walivamia nyumbani kwa Dominic Mgisa mkazi wa kitongoji cha Changómbe na kutafuna ngómbe hao.

Kwa mujibu wa Mgisa, fisi hao waliwatafuna ng’ombe hao na kuwamaliza ndani ya dakika 45.

“Niligundua kuwa mifugo yangu inaliwa na fisi baada ya kutoka nje kujisaidia, niliposogea nikaona fisi, nikaogopa wasije kunidhuru nikarudi ndani,” amesema

Baada ya kuona hivyo Migisa alisema alipiga kelele kuomba msaada kwa majirani lakini hakuna aliyejitokeza kumsaidia kwa kuwa wengi waliwaogopa wanyama hao.
Na Daniel makaka,mwananchi

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527