Leo Jumamosi Mei 12,2018 kumefanyika mchezo wa mpira wa miguu kati ya Shy Town Veteran Sports Club na Shinyanga Veterans.
Katika mchezo huo uliofanyika katika Uwanja wa CCM Kambarage mjini Shinyanga Shy Town Veteran Sports Club walifanikiwa kuichapa Shinyanga Veterans bao 2 - 0 ,mabao yaliyowekwa kimiani na Katoto Mohamed na Abdallah Juma.
Timu ya Shy Town veteran ikiwa tayari kuvaana na Shinyanga Veterans leo katika Uwanja wa CCM Kambarage
Wachezaji wa Shy Town Veteran Sports Club na Shinyanga Veterans kabla ya mchezo.