TAARIFA MUHIMU KUTOKA BODI YA MIKOPO

Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) inawataarifu wanafunzi wanaonufaika na mikopo kuwa  wanatakiwa kuendelea kuingiza taarifa zao kwa njia ya mtandao kupitia http://olas.heslb.go.tz  hadi tarehe 31 Januari, 2018.

Wanafunzi wanufaika wanapaswa kufanya yafuatayo:
•    Tembelea mtandao wa http://olas.heslb.go.tz
•  Fungua kiunganishi cha “Click here to start” kwenye maelezo ya mwanzo ya kukaribisha.
•    Weka namba yako ya mtihani ya Kidato cha Nne na mwaka uliofanya mtihani huo, kwa mfano: S0129.0004.2020
•   Weka namba yako ya akaunti ya Benki kama ilivyowasilishwa HESLB au kama inavyoonekana kwenye “signing sheet”
•    Ingiza neno jipya la siri na ulithibitishe.
•   Baada ya kuthibitisha, ukurasa wa kuweka picha yako “passport size photo” utafunguka.
•    Weka picha yako ya rangi katika ukubwa wa 120×150
•    Wanufaika wapya wa mikopo kwa mwaka wa masomo 2017/2018 hawatahusika kwenye zoezi hili kwa vile taarifa zao ziliwasilishwa wakati wa kuomba mikopo.

Imetolewa na:
Kitengo cha Habari, Elimu na Mawasiliano
BODI YA MIKOPO YA WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU
Tarehe 26/01/2018

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527