Yanga Yapoteza Mchezo wa Pili wa CAF Dhidi ya TP Mazembe,Yaadhibiwa Nyumbani



Juni 28,2016 klabu ya Dar es Salaam Young Africans ilirejea katika uwanja wa Taifa Dar es Salaam ambao ndio uwanja inaoutumia kama uwanja wake wa nyumbani kucheza mechi yake ya pili hatua ya nane bora dhidi ya klabu ya TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.

Katika mchezo huo wa Kundi A lenye timu za Medeama ya Ghana, Mo Bejaia ya Algeria, TP Mazembe ya Kongo na Yanga, umemalizika kwa Yanga kupoteza kwa goli 1-0, goli ambalo limefungwa dakika ya Merveille Bope, TP Mazembe walionekana kucheza kwa umakini na uzoefu mkubwa, kitu ambacho kimeisaidia kupata point tatu.

Kwa matokeo hayo Yanga anakuwa kapoteza mchezo wa pili mfululizo, baada ya mchezo wa kwanza kufungwa kwa goli 1-0 na MO Bejaia ya Algeria, kwa sasa msimamo wa Kundi A unaendelea kuongozwa na TP Mazembe wenye point sita wakifuatiwa na MO Bejaia wenye point tatu, lakini wamezidiwa mchezo na TP Mazembe na Yanga.


Angalia hali ilivyokuwa uwanjani asubuhi



Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527