Katibu Mkuu wa Chama cha ACT-WAZALENDO, Samson Mwigamba Atangaza Kujiuzulu




Katibu Mkuu wa Chama cha ACT - Wazalendo, Samson Mwigamba amejiuzulu nafasi yake ili apate nafasi ya kwenda masomoni Chuo Kikuu cha Kenyatta nchini Kenya.


Kwa mujibu wa ACT-Wazalendo, kamati ya uongozi imekubali maombi ya Mwigamba na kumruhusu kwenda masomoni na kuwa mchakato wa kujaza nafasi hiyo utaanza mara moja.


Naye Mwigamba ameushukuru uongozi wa chama chake kwa ushirikiano waliompatia tangu chama hicho kinaanzishwa. Amesisitiza kwamba bado ni mwanachama na ataendelea kutoa ushirikiano hata akiwa nje ya nchi.


Mwanasiasa huyo anakwenda kusoma shahada ya uzamili katika masuala ya utawala na usimamizi wa biashara (MBA) na baada ya masomo hayo ataendelea na shahada ya uzamivu (PhD).

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post