ASKARI POLISI APORWA BUNDUKI AINA YA SMG NA MAJAMBAZI WALIOKUWA NA NONDO NA MAPANGA


Watu saba wanaosadikiwa kuwa majambazi wakiwa na silaha mbalimbali za jadi, wamempora bunduki aina ya SMG askari polisi PC Shadrack.


Kaimu Kamanda wa Polisi mkoani Dodoma, David Mnyambuga alisema tukio hilo lilitokea juzi saa 2.36 usiku katika ofisi za Kampuni ya Simu za Mkononi ya Halotel, eneo la Medeli.


“Majambazi wapatao saba wakiwa na mapanga na nondo walifika katika ofisi hizo baada ya kutoboa ukuta na kumjeruhi askari kwa mapanga na nondo na kupora silaha aina ya SMG,” alisema.


Kamanda huyo alisema polisi walifanya msako mkali usiku huo na kufanikiwa kuipata silaha hiyo eneo la Mbuyuni.


“Mtu mmoja amekamatwa kuhusiana na tukio hilo na anaendelea kuhojiwa,” alisema.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527