Ajali! TRENI ZAGONGANA,ZAUA NA KUJERUHI WENGI

Treni zilizogongana
Treni zilizogongana
Mtu mmoja ameripotiwa kufariki na wengine 240 kujeruhiwa baada ya treni mbili kugongana katika mji wa Johannesburg nchini Afrika Kusini.
Afisa mmoja wa usalama amesema kuwa ajali hiyo imetokana na msongamano wa wa misafara ya asubuhi.
Afisa huyo ameongeza kwamba treni moja iliyokuwa imeegeshwa katika kituo cha Denver kilichoko kusini mwa mji wa Johannesburg, iligongwa na treni nyingine iliyowasili kutoka jijini Pretoria.

Mlinzi mmoja wa eneo hilo alifariki katika ajali hiyo huku watu wengine 240 wakijeruhiwa na kukimbizwa hospitalini kwa ajili ya matibabu.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527