PROF LIPUMBA KUPIGWA NA POLISI!! BUNGE LAAHIRISHWA TENA JIONI HII,HADI KESHO ASUBUHI



Spika wa Bunge Anna Makinda   jioni  hii  amelazimika kuahirisha  tena  kikao cha Bunge hadi kesho asubuhi  kwa  madai  kuwa  serikali  bado  inajipanga  kutoa  majibu  sahihi  kutokana  na  tukio  la  kupigwa  mabomu  Mwenyekiti  wa  Chama  cha  CUF, Profesa  Ibrahim  Lipumba.

Kuahirishwa  kwa  bunge  kumetokana na vurugu zilizotokea    leo  asubuhi bungeni baada ya kutolewa kwa hoja binafsi kutoka kwa Mbunge na Mwenyekiti wa chama cha NCCR-Mageuzi, James Mbatia kuhusu jeshi la polisi kumshambulia Profesa Ibrahimu Lipumba jana akiwa kwenye maandamano .

Timbwili  zima  la  vurugu  hizo za  Asubuhi  toka  bungeni  liko  hapo  chini  katika  video  iliyopachikwa.
 

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527