Mwanamke mmoja jijini Washington amehukumiwa adhabu ya kifo baada ya kujaribu kuwaua watoto wake watatu kwa kuwakata koromeo ili waache kupiga kelele.
Christina Booth baada
ya kufanya unyama huo, aliwapigia polisi simu na kuwaambia kuwa wanawe
hao wamekua na tabia ya kulia mfululizo bila kunyamaza kitendo
kilichomkasirisha na kuamua kutenda kosa hilo.
Polisi
baada ya kufika eneo la tukio aliwakuta watoto hao ambao mmoja ana
miaka miwili na wengine mapacha wana miaka sita,wakiwa taabani na kuamua
kuwakimbiza hospitali kabla ya kumweka mama yao ndani kutokana na
kufanya unyama huo.