Na mwandishi wetu,Dar
Dar es Salaam, Juni 8, 2026 – Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo ameongoza Kikao cha Baraza la Mawaziri kilichofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam.
Kikao hicho kimewakutanisha Mawaziri wa Serikali kwa ajili ya kujadili na kufanya maamuzi kuhusu masuala mbalimbali ya kitaifa yanayohusu uendeshaji wa Serikali, utekelezaji wa mipango ya maendeleo pamoja na ustawi wa wananchi.
Baraza la Mawaziri ni chombo muhimu cha juu cha Serikali kinachohusika na kutoa mwelekeo wa sera na maamuzi ya kimkakati kwa ajili ya maendeleo ya Taifa.




Social Plugin