Jukwaa la Vijana 'Youth In Action' kutoka GNRC—Tanzania limeendeleza kampeni ya "Kujenga Amani" kwa kushirikiana na taasisi mbalimbali ikiwemo Safari Media Mtwara, Tasa Tanzania na Malunde Media.
Lengo kuu la kampeni hii ni kuwahimiza vijana, hususani maafisa usafirishaji (bodaboda) waliopo mkoani Mtwara, kufanya maamuzi sahihi katika utekelezaji wa shughuli zao ili kuchangia katika kuimarisha amani na sio kuwa chanzo cha uvunjifu wa amani.
Afisa miradi kutoka Shirika la Tasa Tanzania, Betty Chenge amesema kuwa vijana wana nafasi ya kipekee katika kujenga au kubomoa amani.
"Vijana wanapotumika vizuri, hasa katika kipindi hiki cha uchaguzi, watakuwa nguzo muhimu ya maendeleo kwa jamii zao," amesema Chenge.
Kampeni hii inasisitiza kuwa vijana ni wadau muhimu wa maendeleo, na kuwa na uwajibikaji katika jamii kunasaidia kutengeneza mazingira ya amani, uthabiti, na maendeleo endelevu.






Social Plugin