Habari Mpya

6/recent/ticker-posts

RAIS DANIEL CHAPO AWASILI ZANZIBAR KWA ZIARA YA KIKAZI


Rais wa Msumbiji Mheshimiwa Daniel Chapo tayari amewasili Zanzibar akitokea Jijini Dar Es Salaam ambapo akiwa Zanzibar atakua na ziara fupi ya kikazi

Akiwa Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume amepokelewa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Mheshimiwa Hamza Hassan Juma pamoja na viongozi wengine akiwemo Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Nchini Tanzania Mheshimiwa Mahmoud Thabit Kombo

Rais Chapo atakutana na Mwenyeji wake Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt Hussein Ali Mwinyi pamoja na kutembelea kituo cha Uvuvi cha Bahari kuu Fumba

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com