Habari Mpya

6/recent/ticker-posts

Video : ASKOFU MWOMBEKI YUPO URAIANI! ATOKA GEREZANI, ALIFUNGWA JELA MIAKA 30... AFUNGUKA MAZITO ...."RAIS SAMIA"


Askofu wa Kanisa la Emanuel mkoani Shinyanga, Edson Mwombeki, ameibua hisia kali za shukrani na matumaini baada ya kuachiwa huru kutoka gerezani alikokuwa akitumikia kifungo cha miaka 30, ambapo tayari alikuwa ametumikia miaka 10.

Akizungumza mara baada ya kuwasili nyumbani, Askofu Mwombeki amemshukuru Mungu kwa kumuwezesha kupitia kipindi kigumu na hatimaye kupata uhuru wake kupitia msamaha wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan.

Aidha, ametoa shukrani zake za dhati kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa jinsi ambavyo kampeni ya Mama Samia Legal Aid Campaign imekuwa mkombozi kwa wafungwa waliokuwa wamefungwa bila hatia. 

Kupitia kampeni hiyo, kesi nyingi zimefanyiwa mapitio upya na baadhi ya wafungwa, wakiwemo viongozi wa dini kama yeye, wameachiwa huru.

Tazama video kamili hapo chini Askofu Mwombeki akizungumza baada ya kuachiwa huru

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com