
Hii ni siku maalum ya kutambua, kuthamini na kuenzi mchango wa wanahabari katika maendeleo ya taifa, ambapo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika hafla hiyo.
Kaulimbiu ni #UzalendoNdoUjanja, ikihamasisha wanahabari kutumia kalamu zao kwa weledi, maadili na uzalendo wa kweli kwa taifa.
Tuzo hizi zinalenga kutoa motisha kwa wanahabari wanaofanya kazi kwa bidii na ubunifu katika nyanja mbalimbali kama vile habari za uchunguzi, makala bora na habari za maendeleo.
Kwa picha na matukio yanayojiri:
Habari zaidi:
Social Plugin