DC NYAMAHANGA : LIMENI MAZAO YA BIASHARA



Mkuu wa wilaya ya Muleba Dkt Abel Nyamahanga ( aliyekaa katikati)akiwa na baadhi ya viongozi wa vyama vya ushirika

Na Mariam Kagenda _Kagera

Serikali Wilayani Muleba Mkoani Kagera imewataka wakulima kulima mazao ya kibiashara ambayo yatawasaidia kujikwamua kiuchumi na kuondokana na kasumba ya  kilimo cha mazoea ambacho kimekuwa kikisababisha hali ya utegemezi kwenye jamii.

Mkuu wa Wilaya ya Muleba Dkt. Abel Nyamahanga amesema hayo wakati akifunga mafunzo kwa viongozi wa vyama vya ushirika vya matunda na mbogamboga yaliyoandaliwa na tume ya maendeleo ya ushirika (TCDC).

Dkt. Nyamahanga amesema kuwa bado kuna changamoto ya jamii kulima kilimo cha mazoea ambacho hakina tija kwao hivyo kuna haja ya viongozi hao wa ushirika kuhamasisha wakulima kujishughulisha na kilimo cha mazao ya biashara ambacho kitawasaidia kujikwamua kiuchumi.

Kwa upande wake mrajisi msaidizi sehemu ya uhamasishaji na uratibu kutoka tume ya maendeleo ya ushirika TCDC Bw. Ibrahimu Kadudu amesema lengo la mafunzo hayo ni kuwaunganisha wakulima wa mboga mboga  kuwa ushirika mmoja ambao utawasaidia kupata mbegu na masoko ya uhakika kwa wakati mmoja.
Mkuu wa wilaya ya Muleba Dkt Abel Nyamahanga akizungumza na viongozi wa vyama vya ushirika

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post