UZALISHAJI WA MAZAO ASILIA YA BIASHARA YAZIDI KUPAA

Imeelezwa kuwa uzalishaji wa mazao asilia katika mwaka 2023/2024 umeongezeka kutoka tani 1,123,477.92 mwaka 2022/2023 hadi tani 1,260,321.1 sawa na asilimia  78.05 ya lengo la kuzalisha tani 1,614,758.


Hayo yamesemwa na Mhe. Hussein Bashe wakati wa uwasilishaji wa Bajeti ya Wizara ya Kilimo leo Tarehe 02.05/2024 Jijini Dodoma ambapo amesema  ongezeko hilo limechangiwa na uzalishaji wa korosho ambao umefikia tani 254,500 ikilinganishwa na tani 189,113.79 mwaka 2022/2023 sawa na ongezeko la asilimia 63.6 ya lengo la kuzalisha tani 400,000 mwaka 2023/2024.


Aidha Mhe. Bashe amesema uzalishaji wa pamba umefikia tani 282,510 ikilinganishwa na tani 174,486 mwaka 2022/2023 sawa na asilimia 80.7 ya lengo la kuzalisha tani 350,000 mwaka 2023/2024; na uzalishaji wa sukari umefikia tani 392,724 .


Katika uzalishaji wa zao la kahawa amesema uuzalishaji umefikia tani 66,071.8  ikilinganishwa na tani 82,000 mwaka 2022/2023 sawa na asilimia 77.7 ya lengo la kuzalisha tani 85,000; uzalishaji wa pareto  ambao umefikia tani 4,238 ikilinganishwa na tani 3,150 mwaka 2022/2023 sawa na asilimia 121.08 ya lengo la kuzalisha tani 3,500; uzalishaji wa mkonge ambao umefikia tani 56,732.7 ikilinganishwa na tani 48,359.49 mwaka 2022/2023 sawa na asilimia 94.55 ya lengo la kuzalisha tani 60,000.


Pia Mhe. Bashe amesema uzalishaji wa chai ambao umefikia tani 13,525 ikilinganishwa na tani 26,753 mwaka 2022/2023 sawa na asilimia 45 ya lengo la kuzalisha tani 30,000.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post