DKT MPANGO ATOA AGIZO KWA HAZINA ,TAMISEMI KUTUMIA HATI FUNGANI KATIKA KUHARAKISHA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO



Makamu wa Rais Dkt Phillip Mpango akizindua mradi wa kuongeza upatikanaji wa maji kwa wastani wa lita 60 katika Jiji la Tanga na wilaya jirani za Muheza na Mkinga baada ya lita 45 za awali, mradi huo umeanza baada ya uzinduzi wa hati fungani ya Kijani ya Miundombinu ya Maji Tanga katika eneo la Mabayani Jijini Tanga ukiwa na lengo la uboreshaji wa upatikanaji wa maji ambapo unagharama ya zaidi ya Bilioni 53 ambao utazalisha lita milioni 60, kushoto ni Waziri wa Maji Jumaa Aweso akifuatiwa na Mkuu wa Mkoa wa Tanga Waziri Kindamba


Makamu wa Rais Dkt Phillip Mpango akizindua mradi wa kuongeza upatikanaji wa maji kwa wastani wa lita 60 katika Jiji la Tanga na wilaya jirani za Muheza na Mkinga baada ya lita 45 za awali, mradi huo umeanza baada ya uzinduzi wa hati fungani ya Kijani ya Miundombinu ya Maji Tanga katika eneo la Mabayani Jijini Tanga ukiwa na lengo la uboreshaji wa upatikanaji wa maji ambapo unagharama ya zaidi ya Bilioni 53 ambao utazalisha lita milioni 60, kushoto ni Waziri wa Maji Jumaa Aweso akifuatiwa na Mkuu wa Mkoa wa Tanga Waziri Kindamba

Makamu wa Rais Dkt Phillip Mpango akizindua mradi wa kuongeza upatikanaji wa maji kwa wastani wa lita 60 katika Jiji la Tanga na wilaya jirani za Muheza na Mkinga baada ya lita 45 za awali, mradi huo umeanza baada ya uzinduzi wa hati fungani ya Kijani ya Miundombinu ya Maji Tanga katika eneo la Mabayani Jijini Tanga ukiwa na lengo la uboreshaji wa upatikanaji wa maji ambapo unagharama ya zaidi ya Bilioni 53 ambao utazalisha lita milioni 60, kushoto ni Waziri wa Maji Jumaa Aweso akifuatiwa na Mkuu wa Mkoa wa Tanga Waziri Kindamba
Makamu wa Rais Dkt Phillip Mpango akizindua mradi wa kuongeza upatikanaji wa maji kwa wastani wa lita 60 katika Jiji la Tanga na wilaya jirani za Muheza na Mkinga baada ya lita 45 za awali, mradi huo umeanza baada ya uzinduzi wa hati fungani ya Kijani ya Miundombinu ya Maji Tanga katika eneo la Mabayani Jijini Tanga jana ukiwa na lengo la uboreshaji wa upatikanaji wa maji ambapo unagharama ya zaidi ya Bilioni 53 ambao utazalisha lita milioni 60, kushoto ni Waziri wa Maji Jumaa Aweso akifuatiwa na Mkuu wa Mkoa wa Tanga Waziri Kindamba


Makamu wa Rais Dkt Philip Mpango akisalimiana na Waziri wa Afya na Mbunge wa Jimbo la Tanga (CCM) Ummy Mwalimu wa pili kutoka kushoto ni Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Tanga Uwasa Dkt Ally FungoNa Mwandishi wetu.


MAKAMU wa Rais Mhe,Dkt Philip Mpango ameiagiza Ofisi ya usajili wa hazina kama msimamizi wa taasisi na mashirika ya umma nchini wakishirikiana na Ofisi ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tamisemi kuhakikisha wanasimamia Halmashauri nchini kutumia dirisha la hati fungani katika kuharakisha utekelezaji wa miradi ya maendeleo.


Dkt Mpango aliyasema hayo wakati wa ghafla ya uzinduzi wa hatifungani ya kijani ya Mamlaka ya Maji Tanga(Tanga uwasa) na kusema Halmshauri zoye Nchini zitumie dirisha la hati fungani kuharakisha utekelezaji wa miradi ya maendeleo na kutoa nafasi kwa Serikali kujikita kwenye madai mengine ya vipaumbele ambayo hakuna uwezeshwaji wa kifedha.


"Nakuona bwana makopa na ukamwambie bosi wako na Waziri wa Tamisemi hakikisheni mnasimami vizuri taasisi hizo na Halmashauri zote"Alisema Dkt Mpango.



Mbali na agizo hilo pia Dkt Mpango ameiagiza Bodi ya wakurugenzi wa Tanga Uwasa,Menejimenti na Wafanyakazi wote kusimamia vizuri matumizi ya fedha zitakazopatikana kupitia hatifungani ambayo imezinduliwa leo na mapato mengine mtakayokusanya baada ya kukamilisha mradi huo


Aidha alisema nidhamu ya fedha na usimamizi thabiti ndio utakaowezesha kurejesha kwa wakati fedha za wawekezaji wa hatifungani hiyo na Serikali na haitavumilia uzembe wa aina yoyote utakaonekana kukwamisha jitihada za Rais Samia.


"Kwa maneno ya Waziri wa Maji Jumaa aweso kwamba ukimzingua Mama nanyeye atakuzingua sasa shauri yanu"Alisema Dkt Mpango.


Alisema kuwa anatambua kwamba mamlaka za maji kwa kiwango kikubwa zinafanya vzuri na ipo haja ya kuwakumbusha watu wa Tanga Uwasa waongeze ufanisi katika uendeshaji ili urejeshaji wa hatifungani hiyo usiwe sababu ya kuzorota kwa huduma au ongezeko la bei za maji kwa Tanga na Mikoa mingine ambayo itapata nafasi ya kuwa na mradi kama huo.


Makamu huyo wa Rais pia ameiagiza Mamlaka ya Masoko ya mitaji na dhamana (CMSA) kwa kushirikiana na Ofisi ya Rais Mipango na Uwekezaji na wizara ya maji wekeni utararibu na mfumo wa tahadhari ili kufuatilia na kubaini mapema vihatarishi vitakavyoweza kujitokeza baada ya kuzinduliwa kwa hatifungani hiyi.


Dkt Mpango alikwenda mbali zaidi na kusema kwa kuwa urejeshwaji wa fedha hizo ni wa mkupuo baada ya kuiva kwa hatifungani inaweza kuleta changamoto wakati wa kulipa hivyo basi ni vema mjipange mapema na ikiwezekana mfungue mfuko maalumu wa kukusanya kidogo kidogo fedha za marejesho.


"Tuwe na wazo la kibunifu la dira za maji na ninaamini kwa dhati hiyo itasaidia kuongeza ufanisi wa kusanayaji wa mapato na hivyo kuongeza uwezo wa kulipa"Alisema.


Hata hivyo Dkt Philip Mpango alisema hatifungani ambayo imezinduliwa leo ikawe chachu na motisha kwa taasisi na halmashauri nyingine Nchini kutumia njia hiyo kwa ajili ya kupata fedha za miradi ya maendeleo.


Kwaupande wake waziri wa Maji Jumaa Aweso aliishukuru wizara ya Fedha na Mipango kwakufanikisha kupata mradi huo wa hati fungani ambao utasaidia kuongeza ufanisi na upatikanaji wa maji katika jiji la Tanga pamoja na wilaya za Muheza,Pangani na Mkinga,


" Hati fungani itasaidia kuongeza ufanisi wa utendaji kazi na utekelezaji wa miradi ya maji kwenye Wilaya za Tanga jiji,Muheza ,Pangani na mkinga ambapo ,hali ya upatikanaji wa huduma ya maji itapanda ifikapo 2025 hadi asilimia 100 kutoka asilimia 96" alisema Aweso


Alisema wamepata uzoefu wakusimamia miradi mingi ya maji hivyo wanaamini mradi huu wa Hati fungani utatekerezwa na wananchi watapata fursa yakushiriki kwa kiwango kikubwa

Naye Afisa mtendaji wa mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana ( CMSA) Nicodemus Mkama alisema mfumo wa Hatifungani ni sehemu ya Masoko ya mitaji katika Sekta ya fedha inayowezesha upatikanaji wa fedha kwa muda mrefu.

"Fedha za kugharamia shughuli za maendeleo huweza kupatikana kwa kuuza hisa za kampuni ( Shares),hatifungani za kampuni ( corporate Bond) ,hati fungani za Serikali ( Government Bond)na vipande katika mifuko ya uwekezaji wa pamoja ( collective investment scheme) "alisema Mkama

Aliongeza kuwa Taasisi hiyo imepata mafanikio zaidi kwa kipindi cha miaka minne iliyopita ambapo thamani ya uwekezaji katika masoko na mitaji imeongezeka kwa asilimia 31.2 na kufukia shilingi Tirioni 37 .3 katika kipindi kilichoishia January 2024 ikilinganishw na Tirioni 28.4 ya kipindi kilichoishia January 2021,


"Jumla ya mauzo ya hisa na hati fungani katika soko la hisa yameongezeka kwa asilimia 61 .6 na kufikia shilingi tirioni 9.3 kutoka trioni 5.8,vilevile thamani ya mfuko ya uwekezaji wa pamoja imeongezeka kwa asilimia 291.6 na kufikia tirioni 1.9" alisisitiza Mkama

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post