BODI YA TASAC YAUNGA MKONO NA KUPONGEZA JITIHADA ZA TPA KUJENGA BANDARI YA KUHUDUMIA MZIGO MCHAFU KISIWA CHA MGAO














BODI ya Wakurugenzi ya Shirika la Wakala wa Meli Tanzania (TASAC) limeunga mkono na kupongeza jitihada za Mamlaka ya Bandari nchini (TPA) kujenga Bandari ya kuhudumua mizigo Mchafu eneo la Kisiwa -Mgao.

Ujenzi huo unatarajiwa kufanyika katika kisiwa hicho kilichopo katika Halmashauri ya wilaya ya Mtwara Mkoani Mtwara ikiwa ni mkakati wa kusogeza huduma karibu na wananchi.

Hayo yameelezwa na Mwenyekiti wa Bodi hiyo Capt. Mussa Mandia akiwa katika ziara hiyo ya kukagua shughuli mbalimbali zinazofanywa na TASAC chini ya usimamizi wa Bodi hiyo.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post