TPA YAPONGEZWA KUSHIRIKI NA KUDHAMINI MAONESHO YA SITA YA KIMATAIFA YA TEKNOLOJIA YA MADINI MKOANI GEITA.


Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi Prof. Godius Kahyarara ameipongeza TPA kwa kushiriki na kudhamini maonesho ya Sita ya Kimataifa ya Teknolojia ya Madini yaliyofikia tamati leo tarehe 30 Septemba,2023 Katika Viwanja vya EPZ Bombambili Mjini Geita.

Amesisitiza umuhimu wa TPA kufanya Kampeni za Kimasoko ili kupanua Wigo wa biashara na Kampeni za Elimu kwa Umma ili kulinda Taswira ya TPA dhidi upotoshaji unaofifisha umuhimu wa Mamlaka yenye Mchango adhimu kwa Maendeleo ya Uchumi wa Taifa.

Maonesho haya yamefungwa na Makamu wa pili wa Rais Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mhe.Hemed Suleiman Abdullah


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post