MTAALAMU WA MAMBA AKIRI KUNYANYASA KINGONO MAKUMI YA MBWA


Mtaalamu mashuhuri wa mamba wa Uingereza amekiri mashtaka 60 yanayohusiana na ngono na wanyama na nyenzo za unyanyasaji wa watoto.

Mahakama ya Australia ilisikimsikiliza Adam Britton alijirekodi binafsi akiwatesa makumi ya mbwa hadi karibu wote wakafa.

Kisha alichapisha video za matukio hayo mtandaoni, ambapo pia alipata nyenzo za unyanyasaji wa watoto.

Bw Britton ambaye ni mtaalamu wa masuala ya wanyama ambaye amefanya kazi katika BBC na filamu za National Geographic, atahukumiwa baadaye.

Wakati iliposikilizwa kesi yake Mahakama Kuu ya Eneo la Kaskazini (NT) siku ya Jumatatu, waendesha mashtaka waliwasilisha mashitaka dhidi yake.

Mengi ya maelezo ya uhalifu ya Bw Britton ni ya kuogofya na hayawezi kuchapishwa "ni ya kustaajabisha" hakimu alionya watu kuondoka kwenye chumba cha mahakama.

Jaji Mkuu Michael Grant alisema alikuwa na wasiwasi kusikia ukweli wa kesi hiyo kunaweza kusababisha "mshtuko wa neva", kabla ya kuchukua hatua adimu ya kuwaruhusu maafisa wa usalama na maafisa wadogo wa mahakama kuondoka mahakamani, vyombo vya habari vya ndani viliripoti.

Bw Britton alikuwa na "hasira mbaya ya kingono" kwa wanyama tangu mwaka 2014, waendesha mashtaka waliambia mahakama.

Licha ya kuwatumia vibaya mbwa wake kipenzi, aliwalaghai wamiliki wengine wa mbwa kumpa mbwa wao na kuwanyanyasa kingono.

Kati ya mbwa 42 aliowadhulumu katika muda wa miezi 18 kabla ya kukamatwa kwake, 39 walikufa.

Bw Britton amewekwa rumande tangu kukamatwa kwake na atarejea mahakamani kwa ajili ya kusikilizwa kwa hukumu dhidi yake mwezi Desemba.

CHANZO - BBC SWAHILI

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post