RC MTAKA ATEMBELEA BANDA LA TCAA, ASIFU UFANISI WA TAASISI HIYO MAONESHO YA NANENANE MBEYA


Mkuu wa mkoa wa Njombe Mh. Anthony Mtaka (wa pili kushoto)), akizungumza na Meneja Masoko na Uhusiano wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga TCAA Bw. Yesaya Mwakifulefule(wa kwanza kushoto), wakati alipotembelea Katika banda la Mamlaka hiyo kwenye Maonesho ya Kimataifa ya Kilimo ya Nanenane yanayofanyika kwenye viwanja vya John Mwakangale Jijini Mbeya, Katika picha (Kutoka kulia), ni Maureen Swai Afisa Uhusiano na Mawasiliano TCAA, Kassim Ally (Dereva) na Ally Changwila Afisa Uhusiano Mwandamizi TCAA.
Meneja Masokona Uhusiano wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga TCAA Bw. Yesaya Mwakifulefule (kushoto), akimpa maelezo Mwanahabari na Mwana mitindo Mboni Masimba (katikati), wakati alipotembelea Katika banda la Mamlaka hiyo, kwenye Maonesho ya Kimataifa ya Kilimo ya Nanenane yanayofanyika kwenye viwanja vya John Mwakangale Jijini Mbeya.

Mwanahabari na Mwana mitindo Masimba akisaini kitabu cha wageni wakati alipotembelea Katika banda la Mamlaka hiyo kwenye Maonesho ya Kimataifa ya Kilimo ya Nanenane yanayofanyika kwenye viwanja vya John Mwakangale Jijini Mneya kulia ni Maureen Swai Afisa Uhusiano na Mawasiliano TCAA.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post