DIRA YA MAENDELEO YA MWAKA 2025-2050, SERIKALI IWASHIRIKISHE WANANCHI KWENYE MASUALA YA MAENDELEO



********************

NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

KUELEKEA Dira ya Maendeleo ya mwaka 2025-2050, wananchi wameishauri Serikali kuhakikisha inawashirikisha katika kila jambo ambalo lotakuwa na manufaa kwa nchi ili kuondokana na migogoro baina ya Serikali na Wananchi.

Akizungumza leo Augosti 9,2023 Jijini Dar es Salaamwakati wa Semina za Jinsia na Maendeleo zinazoendeshwa na Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP), Bw. Venancy Peter amesema ushirikishwaji wa wananchi utsaidia kuondoa migogoro ambayo imekuwa ikijitokeza mara kwa mara baina ya Serikali na wananchi hasa kwenye masuala ya kiuchumi.

"Tunatumaini Dira ya Maendeleo ijayo ya mwaka 2025 kuelekea 2050 kuona kwamba jamii sasa ishirikishwe kwa kila jambo lenye manufaa kwa taifa letu". Amesema

Kwa upande wake Mshiriki wa Semina, Bi.Subira Abdalah amesema Serikali ijaribu kuzungumza na wananchi kile ambacho wamekiona ili kutengeneza taifa lenye manufaa hapo baadae.





Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post