MWENYEKITI UVCCM KISHAPU AFANYA MKUTANO WA HADHARA KUSIKILIZA KERO ZA VIJANA NA KUZITAFUTIA UFUMBUZI

Na Marco Maduhu,KISHAPU

MWENYEKITI wa Jumuiya ya Umoja wa Vijana ya Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Wilaya ya Kishapu Benard Benson Welema, amefanya Mkutano wa hadhara wa kusikiliza kero za Vijana wilayani humo na kuzitafutia ufumbuzi.

Mkutano huo wa hadhara umefanyika leo Julai 1, 2023 katika Mji wa Mhunze wilayani Kishapu.
Mwenyekiti wa UVCCM Wilaya ya Kishapu Benard Benson Welema akisikiliza kero za vijana.

Amesema amefanya Mkutano huo wa kusikiliza kero mbalimbali ambazo zinawakabili vijana wilayani humo, ili kuzitafutia ufumbuzi, huku akiwataka wachangamkie fursa mbalimbali kupata ajira katika miradi ya kimkakati ambayo inatekelezwa wilayani humo na kujikwamua kiuchumi.
Mwenyekiti wa UVCCM Wilaya ya Kishapu Benard Benson Welema.

“Kero ambazo vijana wenzangu mmeziwasilisha kwenye Mkutano huu tutazifikisha sehemu husika ili zipate kutatuliwa, katika wilaya yetu ya Kishapu kuna miradi ya kimkakati ambayo inatekelezwa changamkieni fursa hizo ili mpate ajira, vibarua na kujikwamua kiuchumi,”amesema Welema.

Aidha, amewataka vijana wilayani humo kuwa Mstari wa mbele kuomba Ajira ambazo zimekuwa zikitangazwa na Halmashauri, ambapo inaonekana muitikio wao kuwa mdogo, pamoja na kuunda vikundi vya ujasiriamali ili wapate mikopo ya asilimia 4 kwa vijana ya halmashauri na kuinuka kiuchumi.
Mwenyekiti wa UVCCM Wilaya ya Kishapu Benard Benson Welema.

“Serikali ilisitisha utoaji wa mikopo asilimia 10 ya mapato ya ndani ya halmashauri baada ya kuona haina tija, na vijana wengi mlikuwa mkikopa lakini hamrejeshi, nawaomba mikopo hii itakapoanza kutolewa itumieni vizuri kufanya uzalishaji na kuwaletea maendeleo na siyo kwenda kuzinyewa Pombe.”amesema Welema.
Katibu wa UVCCM Wilaya ya Kishapu Jamal Namangaya akizungumza kwenye Mkutano huo.

Nao baadhi ya vijana wakiwasilisha kero zao akiwamo Elisha Elias, wameiomba Serikali wilayani humo kwamba fursa mbalimbali ambazo zinatokea zikiwamo za ujenzi na utengenezaji wa samani wawe wanatoa kipaumbele kwanza kwa vijana wilayani humo.

Naye Kijana Michael Mabula, amewasilisha kilio cha ukosefu wa mikopo ya Bodaboda kutoka kwenye Taasisi za kifedha sababu ya kuwa na masharti magumu ya dhamana, na kuwafanya kuendelea kutumikishwa na kushindwa kumiliki bodaboda zao wenyewe.

Diwani wa Songwa Abdul Ngolomole, akizungumza kwenye Mkutano huo, amempongeza Mwenyekiti huyo wa UVCCM wilayani Kishapu kwa kufanya Mkutano wa kusikiliza kero za vijana na kuahidi atashirikiana naye kama diwani kijana ili kuzitafutia ufumbuzi.
Diwani wa Songwa Abdul Ngolomole akizungumza kwenye Mkutano huo.
Mkutano ukiendelea.
Kijana Michael Mabula akiwasilisha baadhi ya kero ambazo zinawakabili vijana wilayani Kishapu
Mkutano ukiendelea.
Elisha Elias akiwasilisha baadhi ya kero ambazo zinawakabili vijana wilayani Kishapu.
Mkutano ukiendelea.
Mkutano ukiendelea.
Mkutano ukiendelea.
Mkutano ukiendelea.
Mkutano ukiendelea.
Mkutano ukiendelea.
Mkutano ukiendelea.
Mkutano ukiendelea.
Baadhi ya akina Mama wakiwa kwenye Mkutano wa Mwenyekiti wa UVCCM wilayani Kishapu.
Mkutano ukiendelea.
Mkutano ukiendelea.
Mkutano ukiendelea.
Mkutano ukiendelea.
Mkutano ukiendelea.
Mkutano ukiendelea.
Akina Mama wakiimba nyimbo za CCM kwenye Mkutano wa Mwenyekiti wa UVCCM wilayani Kishapu.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post