MO MLIMWENGU AAHIDI KUFANYA MAAJABU CCM MULEBA



Mo Mlimwengu

Na Mwandishi wetu _ Muleba

Katibu Hamasa wa vijana na chipukizi Umoja wa vijana CCM wilaya ya Muleba mkoani Kagera Mo Mlimwengu amesema atahakikisha anashirikiana na vijana ili kuimarisha jumuia hiyo.


Mo Mlimwengu amesema hayo ikiwa ni siku chache zimepita tangu achaguliwe na wajumbe wa Jumuiya hiyo kuwa katibu hamasa wa vijana na chipukizi katika wilaya ya Muleba .


Amesema kuwa alipoambiwa kuhusu nafasi hii alijitafakari kwanza ili aone kama anaweza wanza aliaangalia majukumu ya kiongozi wa CCM ni yapi? akabaini kuna mambo kama matatu ambayo ni pamoja na kukijenga chama.


"Wakati Baraza linanipitisha kuna watu walikuwa tayari kufanya lolote wahakikishe Mo Mlimwengu anakuwa mshindi lakini kuna watu hawakuwa tayari kuona napata hiyo nafasi. Hao wachache ambao hawakuwa tayari ndio walionipa deni kubwa kuhakikisha nafanya kama ipasavyo",amesema.


Amewashukuru wajumbe wa Baraza is vijana wilaya ya Muleba kwa kuonyesha upendo wa hali ya juu kwake na kusema wamesimama imara kwa ajili ya masrahi ya vijana wa Muleba .

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post