YANGA SC YAITANDIKA SINGIDA BIG STARS 2-0, YAUSOGELEA UBINGWA


NA EMMANUEL MBATILO

KLABU ya Yanga imeendelea kuusogelea ubingwa wa Ligi ya NBC mara baada ya kufanikiwa kuichapa Singida Big Star kwa mabao 2-0, mchezo ambao ulipigwa kwenye dimba la Liti mkoani Singida.

Yanga ilianza kupata bao la mapema kupitia kwa Aziz Ki huku bao la pili likifungwa na Clement Mzize na kuisadia timu yao kuongoza katika kipindi cha kwanza kwa mbao 2-0.

Kipindi cha pili Yanga ilirudi ikiwa inahitaji mabao zaidi kwani ilikuwa inalisakama lango la mpinzani japokuwa hawakufanikiwa kuongeza mabao mengine mpaka dakika 90 mpira kumalizika matokeo yakiwa 2-0.

Yanga Sc sasa inaendelea kukaa kileleni mwa ligi ikiwa na pointi 71 wakiwa wameshuka dimbani mara 27 huku nafasi ya pili akiwa bado inashikwa na timu ya Simba ambao hapo jana walialzimishwa sare na Namungo Fc na kuwafanya wapinzani wao Yanga kukaribia ubingwa wa ligi hiyo.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments